Zaburi26
Listen to this chapter
0:00
0:00
1
Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Bwana bila kusitasita.
2
Ee Bwana, unijaribu, unipime, uuchunguze moyo wangu na mawazo yangu;
3
kwa maana upendo wako uko mbele yangu daima, nami natembea siku zote katika kweli yako.
4
Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
5
ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
6
Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
7
nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
8
Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, mahali ambapo utukufu wako hukaa.
9
Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,
10
ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.
11
Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.
12
Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Options
Study Note