Zaburi126
Listen to this chapter
0:00
0:00
Kukumbuka kwa Furaha Kurejeshwa
1
Wimbo wa kwenda juu. Bwana alipowarejeza mateka Sayuni, tulikuwa kama watu walioota ndoto.
2
Vinywa vyetu vilijaa kicheko, ndimi zetu zilijaa nyimbo za shangwe. Ndipo iliposemwa miongoni mwa mataifa, “Bwana amewatendea mambo makuu.”
3
Bwana ametutendea mambo makuu, nasi tumejaa furaha.
Maombi ya Kurejeshwa Kikamilifu na Mavuno
4
Ee Bwana, turejeshee watu wetu waliotekwa, kama vijito katika Negebu.
5
Wapandao kwa machozi watavuna kwa nyimbo za shangwe.
6
Yeye azichukuaye mbegu zake kwenda kupanda, huku akilia, atarudi kwa nyimbo za shangwe, akichukua miganda ya mavuno yake.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Reading Width chars
Options
Study Note