Zaburi120
Listen to this chapter
0:00
0:00
Kilio cha Kuomba Wokovu
1
Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
2
Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
Hatima ya Wadanganyifu
3
Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
4
Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
Kuomboleza Uhamishoni Kati ya Watu Wenye Uadui
5
Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
6
Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
7
Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Reading Width chars
Options
Study Note