Skip to content
Warumi 11:25-29

Warumi 11:25-29

25
Ndugu zangu, ili msije mkajidai kuwa wenye hekima kuliko mlivyo, nataka mfahamu siri hii: Ugumu umewapata Israeli kwa sehemu hadi idadi ya watu wa Mataifa watakaoingia itimie.
26
Hivyo Israeli wote wataokolewa. Kama ilivyoandikwa: “Mkombozi atakuja kutoka Sayuni; ataondoa kutokumcha Mungu katika Yakobo.
27
Hili ndilo agano langu nao nitakapoziondoa dhambi zao.”
28
Kwa habari ya Injili, wao ni adui wa Mungu kwa ajili yenu, lakini kuhusu kule kuteuliwa kwao ni wapendwa, kwa ajili ya mababa zao wa zamani,
29
kwa maana akishawapa watu karama, Mungu haziondoi, wala wito wake.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options