Zaburi 94:7-11
7
Nao husema, “Bwana haoni, Mungu wa Yakobo hafahamu.”
8
Sikizeni, enyi wajinga miongoni mwa watu; enyi wapumbavu, lini mtakuwa na hekima?
9
Je, aliyeweka sikio asisikie? Aliyeumba jicho asione?
10
Je, anayeadhibisha mataifa asiadhibu? Je, awafundishaye wanadamu asiwe na maarifa?
11
Bwana anajua mawazo ya mwanadamu; anajua kwamba ni ubatili.
Settings