Zaburi 94:1-7
1
Ee Bwana, ulipizaye kisasi, Ee Mungu ulipizaye kisasi, uangaze sasa.
2
Ee Mhukumu wa dunia, inuka, uwalipize wenye kiburi kama wanavyostahili.
3
Hata lini, waovu, Ee Bwana, hata lini waovu watashangilia?
4
Wanamimina maneno ya kiburi, watenda mabaya wote wamejaa majivuno.
5
Ee Bwana, wanawaponda watu wako, wanawaonea urithi wako.
6
Wanamchinja mjane na mgeni, na kuwaua yatima.
7
Nao husema, “Bwana haoni, Mungu wa Yakobo hafahamu.”
Settings