Zaburi 94:3-7
3
Hata lini, waovu, Ee Bwana, hata lini waovu watashangilia?
4
Wanamimina maneno ya kiburi, watenda mabaya wote wamejaa majivuno.
5
Ee Bwana, wanawaponda watu wako, wanawaonea urithi wako.
6
Wanamchinja mjane na mgeni, na kuwaua yatima.
7
Nao husema, “Bwana haoni, Mungu wa Yakobo hafahamu.”