Zaburi 94:17-19
17
Kama Bwana asingelinisaidia upesi, ningelikuwa ninaishi katika ukimya wa kifo.
18
Niliposema, “Mguu wangu unateleza,” Ee Bwana, upendo wako ulinishikilia.
19
Wakati wasiwasi ulipokuwa mwingi ndani yangu, faraja yako ilinipa furaha nafsini mwangu.