Zaburi 92:7-15
7
ingawa waovu huchipua kama majani na wote watendao mabaya wanastawi, wataangamizwa milele.
8
Bali wewe, Ee Bwana, utatukuzwa milele.
9
Ee Bwana, hakika adui zako, hakika adui zako wataangamia. Wote watendao mabaya watatawanyika.
10
Umeitukuza pembe yangu kama ile ya nyati dume, mafuta mazuri yamemiminwa juu yangu.
11
Macho yangu yamewaona adui zangu wakishindwa, masikio yangu yamesikia maangamizi ya adui zangu waovu.
12
Wenye haki watastawi kama mtende, watakuwa kama mwerezi wa Lebanoni,
13
waliopandwa katika nyumba ya Bwana, watastawi katika nyua za Mungu wetu.
14
Wakati wa uzee watakuwa bado wanazaa matunda, watakuwa wabichi tena wamejaa nguvu,
15
wakitangaza, “Bwana ni mkamilifu; yeye ni Mwamba wangu, na ndani yake hamna uovu.”
Settings