Zaburi 92:5-9
5
Ee Bwana, tazama jinsi yalivyo makuu matendo yako, tazama jinsi yalivyo ya kina mawazo yako!
6
Mjinga hafahamu, mpumbavu haelewi,
7
ingawa waovu huchipua kama majani na wote watendao mabaya wanastawi, wataangamizwa milele.
8
Bali wewe, Ee Bwana, utatukuzwa milele.
9
Ee Bwana, hakika adui zako, hakika adui zako wataangamia. Wote watendao mabaya watatawanyika.
Settings