Makao ya Waaminifu
Zaburi 91:9-13
9
Kama ukimfanya Aliye Juu Sana kuwa makao yako: naam, Bwana ambaye ni kimbilio langu,
10
basi hakuna madhara yatakayokupata wewe, hakuna maafa yataikaribia hema yako.
11
Kwa kuwa atawaagiza malaika zake kwa ajili yako, wakulinde katika njia zako zote.
12
Mikononi mwao watakuinua, ili usijikwae mguu wako kwenye jiwe.
13
Utawakanyaga simba na nyoka wakali, simba mkubwa na nyoka utawaponda kwa miguu.
Settings