Zaburi 91:3-10
3
Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji, na maradhi ya kuambukiza ya kuua.
4
Atakufunika kwa manyoya yake, chini ya mbawa zake utapata kimbilio, uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.
5
Hutaogopa vitisho vya usiku, wala mshale urukao mchana,
6
wala maradhi ya kuambukiza yanayonyemelea gizani, wala tauni iharibuyo adhuhuri.
7
Ijapo watu elfu wataangukia kando yako, kumi elfu mkono wako wa kuume, lakini haitakukaribia wewe.
8
Utatazama tu kwa macho yako na kuona adhabu ya waovu.
9
Kama ukimfanya Aliye Juu Sana kuwa makao yako: naam, Bwana ambaye ni kimbilio langu,
10
basi hakuna madhara yatakayokupata wewe, hakuna maafa yataikaribia hema yako.
Settings