Zaburi 9:15-18
15
Mataifa wameanguka kwenye shimo walilolichimba, miguu yao imenaswa kwenye wavu waliouficha.
16
Bwana anajulikana kwa haki yake, waovu wamenaswa katika kazi za mikono yao.
17
Waovu wataishia kuzimu, naam, mataifa yote wanaomsahau Mungu.
18
Lakini mhitaji hatasahaulika siku zote, wala matumaini ya walioonewa hayatapotea.
Settings