Skip to content
Zaburi 89:38-45

Zaburi 89:38-45

38
Lakini wewe umemkataa, umemdharau, umemkasirikia sana mpakwa mafuta wako.
39
Umelikana agano lako na mtumishi wako, na umeinajisi taji yake mavumbini.
40
Umebomoa kuta zake zote, na ngome zake zote umezifanya kuwa magofu.
41
Wote wapitao karibu wamemnyangʼanya mali zake; amekuwa dharau kwa jirani zake.
42
Umeutukuza mkono wa kuume wa adui zake, umewafanya watesi wake wote washangilie.
43
Umegeuza makali ya upanga wake, na hukumpa msaada katika vita.
44
Umeikomesha fahari yake, na kukiangusha kiti chake cha enzi.
45
Umezifupisha siku za ujana wake, umemfunika kwa vazi la aibu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options