Zaburi 89:30-34
30
“Kama wanae wataacha amri yangu na wasifuate sheria zangu,
31
kama wakihalifu maagizo yangu na kutoshika amri zangu,
32
nitaadhibu dhambi yao kwa fimbo, uovu wao kwa kuwapiga,
33
lakini sitauondoa upendo wangu kwake, wala sitausaliti uaminifu wangu kamwe.
34
Mimi sitavunja agano langu wala sitabadili lile ambalo midomo yangu imelitamka.
Settings