Skip to content
Zaburi 89:29-37

Zaburi 89:29-37

29
Nitaudumisha uzao wake milele, kiti chake cha enzi kama mbingu zinavyodumu.
30
“Kama wanae wataacha amri yangu na wasifuate sheria zangu,
31
kama wakihalifu maagizo yangu na kutoshika amri zangu,
32
nitaadhibu dhambi yao kwa fimbo, uovu wao kwa kuwapiga,
33
lakini sitauondoa upendo wangu kwake, wala sitausaliti uaminifu wangu kamwe.
34
Mimi sitavunja agano langu wala sitabadili lile ambalo midomo yangu imelitamka.
35
Mara moja na kwa milele, nimeapa kwa utakatifu wangu, nami sitamdanganya Daudi:
36
kwamba uzao wake utaendelea milele, na kiti chake cha enzi kitadumu mbele zangu kama jua;
37
kitaimarishwa milele kama mwezi, shahidi mwaminifu angani.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options