Zaburi 89:28-34
28
Nitadumisha upendo wangu kwake milele, na agano langu naye litakuwa imara.
29
Nitaudumisha uzao wake milele, kiti chake cha enzi kama mbingu zinavyodumu.
30
“Kama wanae wataacha amri yangu na wasifuate sheria zangu,
31
kama wakihalifu maagizo yangu na kutoshika amri zangu,
32
nitaadhibu dhambi yao kwa fimbo, uovu wao kwa kuwapiga,
33
lakini sitauondoa upendo wangu kwake, wala sitausaliti uaminifu wangu kamwe.
34
Mimi sitavunja agano langu wala sitabadili lile ambalo midomo yangu imelitamka.
Settings