Zaburi 89:20-29
20
Nimemwona Daudi, mtumishi wangu, na nimemtia mafuta yangu matakatifu.
21
Kitanga changu kitamtegemeza, hakika mkono wangu utamtia nguvu.
22
Hakuna adui atakayemtoza ushuru, hakuna mtu mwovu atakayemwonea.
23
Nitawaponda adui zake mbele zake na kuwaangamiza watesi wake.
24
Upendo wangu mkamilifu utakuwa pamoja naye, kwa Jina langu pembe yake itatukuzwa.
25
Nitauweka mkono wake juu ya bahari, mkono wake wa kuume juu ya mito.
26
Naye ataniita kwa sauti, ‘Wewe ni Baba yangu, Mungu wangu, Mwamba na Mwokozi wangu.’
27
Nitamteua pia awe mzaliwa wangu wa kwanza, aliyetukuka kuliko wafalme wote wa dunia.
28
Nitadumisha upendo wangu kwake milele, na agano langu naye litakuwa imara.
29
Nitaudumisha uzao wake milele, kiti chake cha enzi kama mbingu zinavyodumu.
Settings