Zaburi 84:8-12
8
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, sikia maombi yangu; nisikilize, Ee Mungu wa Yakobo.
9
Ee Mungu, uitazame ngao yetu, mtazame kwa wema mpakwa mafuta wako.
10
Siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu mahali pengine; afadhali ningekuwa bawabu katika nyumba ya Mungu wangu kuliko kukaa katika mahema ya waovu.
11
Kwa kuwa Bwana ni jua na ngao, Bwana hutoa wema na heshima; hakuna kitu chema anachowanyima wale ambao hawana hatia.
12
Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, heri ni mtu yule anayekutumaini wewe.
Settings