Zaburi 83:16-18
16
Funika nyuso zao kwa aibu ili watu walitafute jina lako, Ee Bwana.
17
Wao na waaibishwe na kufadhaishwa milele, na waangamie kwa aibu.
18
Hebu wajue kwamba wewe, ambaye jina lako ni Bwana, kwamba wewe peke yako ndiwe Uliye Juu Sana ya dunia yote.