Skip to content
Zaburi 83:13-18

Zaburi 83:13-18

13
Ee Mungu wangu, wapeperushe kama mavumbi ya kisulisuli, kama makapi yapeperushwayo na upepo.
14
Kama vile moto uteketezavyo msitu au mwali wa moto unavyounguza milima,
15
wafuatilie kwa tufani yako na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
16
Funika nyuso zao kwa aibu ili watu walitafute jina lako, Ee Bwana.
17
Wao na waaibishwe na kufadhaishwa milele, na waangamie kwa aibu.
18
Hebu wajue kwamba wewe, ambaye jina lako ni Bwana, kwamba wewe peke yako ndiwe Uliye Juu Sana ya dunia yote.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options