Zaburi 78:19-25
19
Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
20
Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
21
Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
22
kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
23
Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
24
akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
25
Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
Settings