Zaburi 74:3-5
3
Geuza hatua zako kuelekea magofu haya ya kudumu, uharibifu wote huu ambao adui ameuleta pale patakatifu.
4
Adui zako wamenguruma pale ulipokutana nasi, wanaweka bendera zao kama alama.
5
Walifanya kama watu wanaotumia mashoka kukata kichaka cha miti.