Zaburi 68:7-14
7
Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako, ulipopita nyikani,
8
dunia ilitikisika, mbingu zikanyesha mvua, mbele za Mungu, Yule wa Sinai, mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.
9
Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.
10
Ee Mungu, watu wako waliishi huko, nawe kwa wingi wa utajiri wako uliwapa maskini mahitaji yao.
11
Bwana alitangaza neno, waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:
12
“Wafalme na majeshi walikimbia upesi, watu waliobaki kambini waligawana nyara.
13
Hata ulalapo katikati ya mioto ya kambini, mabawa ya njiwa wangu yamefunikwa kwa fedha, manyoya yake kwa dhahabu ingʼaayo.”
14
Wakati Mwenyezi alipowatawanya wafalme katika nchi, ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.
Settings