Zaburi 65:10-13
10
Umeilowesha mifereji yake na kusawazisha kingo zake; umeilainisha kwa manyunyu na kuibariki mimea yake.
11
Umeuvika mwaka taji ya baraka, magari yako yanafurika kwa wingi.
12
Mbuga za majani za jangwani umezineemesha; vilima vimevikwa furaha.
13
Penye nyanda za malisho pamejaa makundi ya wanyama, na mabonde yamepambwa kwa mavuno; vyote vinashangilia kwa furaha na kuimba.
Settings