Skip to content
Zaburi 61:3-4

Zaburi 61:3-4

3
Kwa kuwa umekuwa kimbilio langu, ngome imara dhidi ya adui.
4
Natamani kukaa hemani mwako milele, na kukimbilia chini ya uvuli wa mbawa zako.

See also

Where else Scripture says this.

  • Mithali 18:10

    Jina la Bwana ni ngome imara, wenye haki huikimbilia na kuwa salama.
    from verse 3
  • Zaburi 23:6

    Hakika wema na upendo vitanifuata siku zote za maisha yangu, nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele.
    from verse 4
  • Zaburi 27:4

    Jambo moja ninamwomba Bwana, hili ndilo ninalolitafuta: niweze kukaa nyumbani mwa Bwana siku zote za maisha yangu, niutazame uzuri wa Bwana na kumtafuta hekaluni mwake.
    from verse 4
  • Zaburi 17:8

    Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
    from verse 4
  • Zaburi 62:7

    Wokovu wangu na heshima yangu viko kwa Mungu, ndiye mwamba wangu wenye nguvu na kimbilio langu.
    from verse 3
  • Zaburi 91:4

    Atakufunika kwa manyoya yake, chini ya mbawa zake utapata kimbilio, uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.
    from verse 4
  • Zaburi 140:7

    Ee Bwana Mwenyezi, Mwokozi wangu mwenye nguvu, unikingaye kichwa changu siku ya vita:
    from verse 3
  • Zaburi 15:1

    Zaburi ya Daudi. Bwana, ni nani awezaye kukaa katika Hekalu lako? Nani awezaye kuishi katika mlima wako mtakatifu?
    from verse 4
  • Zaburi 57:1

    Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni. Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie, kwa maana nafsi yangu inakukimbilia. Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia mpaka maafa yapite.
    from verse 4
  • Zaburi 63:7

    Kwa sababu wewe ndiwe msaada wangu, chini ya uvuli wa mbawa zako naimba.
    from verse 4
  • 2 Wakorintho 1:10

    Yeye aliyetuokoa kwenye hatari kubwa ya kifo na atatuokoa tena. Kwake yeye tumeweka tumaini letu kwamba ataendelea kutuokoa.
    from verse 3
  • Zaburi 18:2

    Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu, Mungu wangu ni mwamba, ambaye kwake ninakimbilia. Yeye ni ngao yangu na pembe ya wokovu wangu, ngome yangu.
    from verse 3
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options