Zaburi 55:1-5
1
Kwa mwimbishaji. Na ala za uimbaji. Utenzi wa Daudi. Ee Mungu, sikiliza maombi yangu, wala usidharau hoja yangu.
2
Nisikie na unijibu. Mawazo yangu yananisumbua na nimehangaishwa
3
kwa sauti ya adui, kwa kukaziwa macho na waovu, kwa sababu wananiletea mateso juu yangu na kunitukana kwa hasira zao.
4
Moyo wangu umejaa uchungu, hofu ya kifo imenishambulia.
5
Woga na kutetemeka vimenizunguka, hofu kuu imenigharikisha.
Settings