Zaburi 48:3-8
3
Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
4
Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
5
walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
6
Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
7
Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
8
Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
Settings