Zaburi 48:1-8
1
Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
2
Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
3
Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
4
Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
5
walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
6
Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
7
Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
8
Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
Settings