Zaburi 38:12-14
12
Wale wanaotafuta uhai wangu wanatega mitego yao, wale ambao wangetaka kunidhuru huongea juu ya maangamizi yangu; hufanya shauri la hila mchana kutwa.
13
Mimi ni kama mtu kiziwi, asiyeweza kusikia, ni kama bubu, asiyeweza kufungua kinywa chake,
14
nimekuwa kama mtu asiyesikia, ambaye kinywa chake hakiwezi kutoa jibu.
Settings