Zaburi 37:3-6
3
Mtumaini Bwana na utende yaliyo mema; Kaa katika nchi ukafurahie malisho salama.
4
Jifurahishe katika Bwana naye atakupa haja za moyo wako.
5
Mkabidhi Bwana njia yako, mtumaini yeye, naye atatenda hili:
6
Yeye atafanya haki yako ingʼae kama mapambazuko, na hukumu ya shauri lako kama jua la adhuhuri.
Settings