Skip to content
Zaburi 37:1-6

Zaburi 37:1-6

1
Zaburi ya Daudi. Usisumbuke kwa ajili ya watendao maovu, wala usiwaonee wivu watendao mabaya,
2
kwa maana kama majani watanyauka mara, kama mimea ya kijani watakufa mara.
3
Mtumaini Bwana na utende yaliyo mema; Kaa katika nchi ukafurahie malisho salama.
4
Jifurahishe katika Bwana naye atakupa haja za moyo wako.
5
Mkabidhi Bwana njia yako, mtumaini yeye, naye atatenda hili:
6
Yeye atafanya haki yako ingʼae kama mapambazuko, na hukumu ya shauri lako kama jua la adhuhuri.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options