Zaburi 34:3-6
3
Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
4
Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
5
Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
6
Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.