Zaburi 33:12-19
12
Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.
13
Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini na kuwaona wanadamu wote;
14
kutoka maskani mwake huwaangalia wote wakaao duniani:
15
yeye ambaye huumba mioyo yao wote, ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.
16
Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake; hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.
17
Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu, licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.
18
Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao, kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,
19
ili awaokoe na mauti, na kuwahifadhi wakati wa njaa.
Settings