Zaburi 30:1-3
1
Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi. Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu.
2
Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.
3
Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti.