Zaburi 30:1-5
1
Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi. Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu.
2
Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.
3
Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti.
4
Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu.
5
Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha.
Settings