Zaburi 22:12-15
12
Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.
13
Simba wangurumao wanaorarua mawindo yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.
14
Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.
15
Nguvu zangu zimekauka kama kigae, ulimi wangu umegandamana na kaakaa la kinywa changu, kwa sababu umenilaza katika mavumbi ya kifo.
Settings