Zaburi 2:4-9
4
Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
5
Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
6
“Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
7
Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
8
Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
9
Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
Settings