Zaburi 18:43-45
43
Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu; umenifanya kuwa kiongozi wa mataifa, watu ambao sikuwajua wananitumikia.
44
Mara wanisikiapo hunitii, wageni hunyenyekea mbele yangu.
45
Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.