Skip to content
Zaburi 18:37-43

Zaburi 18:37-43

37
Niliwafuatia adui zangu na nikawapata, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
38
Niliwaseta hata hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
39
Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
40
Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
41
Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
42
Niliwaponda kama mavumbi yanayopeperushwa na upepo; niliwamwaga nje kama tope barabarani.
43
Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu; umenifanya kuwa kiongozi wa mataifa, watu ambao sikuwajua wananitumikia.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options