Zaburi 18:37-42
37
Niliwafuatia adui zangu na nikawapata, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
38
Niliwaseta hata hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
39
Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
40
Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
41
Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
42
Niliwaponda kama mavumbi yanayopeperushwa na upepo; niliwamwaga nje kama tope barabarani.
Settings