Zaburi 18:32-36
32
Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
33
Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
34
Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
35
Hunipa ngao yako ya ushindi, nao mkono wako wa kuume hunitegemeza, unajishusha chini ili kuniinua.
36
Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
Settings