Zaburi 147:16-18
16
Anatandaza theluji kama sufu na kutawanya umande kama majivu.
17
Huvurumisha mvua yake ya mawe kama changarawe. Ni nani awezaye kustahimili ukali wa baridi yake?
18
Hutuma neno lake na kuviyeyusha, huvumisha upepo wake, nayo maji hutiririka.