Zaburi 147:15-18
15
Hutuma amri yake duniani, neno lake hukimbia kasi.
16
Anatandaza theluji kama sufu na kutawanya umande kama majivu.
17
Huvurumisha mvua yake ya mawe kama changarawe. Ni nani awezaye kustahimili ukali wa baridi yake?
18
Hutuma neno lake na kuviyeyusha, huvumisha upepo wake, nayo maji hutiririka.