Zaburi 145:1-7
1
Wimbo wa Sifa. Wa Daudi. Nitakutukuza wewe, Mungu wangu Mfalme, nitalisifu jina lako milele na milele.
2
Kila siku nitakusifu na kulitukuza jina lako milele na milele.
3
Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, ukuu wake haupimiki.
4
Kizazi kimoja kitasifia kazi zako kwa kizazi kingine, watasimulia matendo yako makuu.
5
Watasema juu ya utukufu wa fahari ya ukuu wako, nami nitatafakari juu ya kazi zako za ajabu.
6
Watasimulia uwezo wa kazi zako za kutisha, nami nitatangaza matendo yako makuu.
7
Wataadhimisha wema wako mwingi, na wataimba kwa shangwe juu ya haki yako.
Settings