Zaburi 132:13-17
13
Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
14
“Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
15
Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
16
Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
17
“Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
Settings