Zaburi 132:11-18
11
Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
12
kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
13
Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
14
“Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
15
Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
16
Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
17
“Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
18
Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”
Settings