Zaburi 130:1-4
1
Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
2
Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
3
Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
4
Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.