Zaburi 12:2-4
2
Kila mmoja humwambia jirani yake uongo; midomo yao ya hila huzungumza kwa udanganyifu.
3
Bwana na akatilie mbali midomo yote ya hila na kila ulimi uliojaa majivuno,
4
ule unaosema, “Kwa ndimi zetu tutashinda; midomo ni mali yetu, bwana wetu ni nani?”