Skip to content
Zaburi 119:1-8

Zaburi 119:1-8

1
Heri wale walio waadilifu katika njia zao, wanaoenenda katika sheria ya Bwana.
2
Heri wale wanaozishika shuhuda zake, wamtafutao kwa moyo wao wote.
3
Wasiofanya lolote lililo baya, wanaoenenda katika njia zake.
4
Umetoa maagizo yako ili tuyatii kwa ukamilifu.
5
Laiti mwenendo wangu ungekuwa imara katika kuyatii maagizo yako!
6
Hivyo mimi sitaaibishwa ninapozingatia amri zako zote.
7
Nitakusifu kwa moyo mnyofu ninapojifunza sheria zako za haki.
8
Nitayatii maagizo yako; usiniache kabisa.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options